Kwa Simba hii, Kununa uwe na sababu
KAMA ni sifa, basi hao Simba wamezidi sasa na kama ni kuwakera wapinzani wao, basi wanawakeraa kweli. Ndio, achana na mechi yao usiku wa jana wakati wakimkaribisha jijini Dar es Salaam Kocha Mwinyi Zahera na chama lake la Gwambina, unaambiwa kikosi cha Kocha Sven Vandenbroeck ni moto ile mbaya hasa safu yake ya mbele.
Comments (0)