HATMA SAKATA LA MORRISON KUJULIKANA LEO
Msomaji wa Yanganews Blog:Jana kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF, chini ya Mwenyekiti wake, Elias Mwanjala, ilikutana kupitia mambo mbalimbali ikiwamo malalamiko ya Yanga iliyoyatoa hivi karibuni kupitia kwa Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Frederick Mwakalebela, kuwa mkataba kati ya Simba na Morrison unadosari kwa kile alichodai kuwa hauna saini yoyote ya kiongozi wa klabu ya Simba
Mwenyekiti huyo alimwambia chanzo chetu jana kuwa, tayari wamepitia malalamiko hayo na leo kila kitu kitawekwa hadharani kuhusu hatima waliyofikia
,,
Comments (0)